Latest Post

Mteja wa Bank of Africa-Tanzania (BOA),Bw.Dolvin Salvatory Olomi, kutoka Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro,amebahatika  kuibuka mshindi wa jumla wa shilingi milioni 5 kupitia kampeni iliyomalizika iitwayo “Miamala ni Fursa.”

Meneja wa Tawi la Bank of Africa Tanzania tawi la  Moshi, Bi. Mpoki Mwanjala akikabidhi hundi ya mfano ya shilingi milioni 5 kwa Bw. Dolvin Olomi, mshindi wa kampeni ya Miamala ni Fursa, baada ya kutangazwa mshindi wa kampeni hiyo katika hafla iliyofanyika katika tawi la Benki hiyo.

Kampeni hiyo, iliyoanza Juni hadi Septemba 2025, iliwezesha zaidi ya washindi 60 nchi nzima kujinyakulia  zawadi, huku wateja wakipata zawadi za kila wiki za Shilingi 50,000 kwa kutumia huduma za kidigitali zinazotolewa na Benki. Kampeni ilifikia kilele kwa droo kubwa ya mwisho, ambayo ilitoa zawadi kubwa  ya Shilingi 5 milioni kwa mtumiaji bora wa huduma ya kidijitali—aliyetangazwa rasmi kuwa mshindi mkuu kupitia droo ya bahati nasibu hiyo.

"Kushinda Shilingi milioni 5  kwa kutumia  huduma ya benki kwa njia ya simu kumebadilisha maisha yangu," alisema Bw Olomi, ambaye alitoa shukurani zake za dhati kwa Bank of Africa-Tanzania,  kwa kukuza ushirikishwaji wa kifedha kupitia kampeni za kibunifu na zenye kuleta manufaa kwa wateja wake.

Kampeni ya “Miamala ni Fursa” ilizinduliwa Juni 4, 2025, na ilianzishwa ili kuhimiza utumiaji wa huduma za benki kidijitali kwa kufanya miamala ya kila siku, ikijumuisha uhamishaji wa fedha kutoka benki  kwa matumizi mbalimbali, kufanya malipo ya ankra,kununua   muda wa maongezi au umeme. Kampeni hii ni sehemu ya dhamira pana ya benki ya kuunga mkono  ajenda ya Serikali ya Tanzania ya  matumizi ya huduma za kidijitali na kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma za fedha kwa wote.

Ofisa Mkuu wa Huduma za Kidijitali wa Bank Of Africa-Tanzania ,Lameck Mushi alisema: "Mafanikio ya kampeni ni ishara tosha kwamba Watanzania wako tayari kutumia huduma za kibenki za kidijitali ambazo ni rahisi, zinaweza kufikiwa na ni zenye manufaa. Kupunguza ada ya uhamisho kutoka benki kwa matumizi mbalimbali kwa zaidi ya asilimia 50% na kufanikisha kuongeza matumizi ya huduma za kifedha kwa njia ya simu kufanya miamala, na msisimko wa kushinda zawadi uliongeza zaidi."

Bw Mushi aliongeza: "Iwe unaishi maeneo ya mjini au vijijini, matumizi ya huduma za Kibenki kwa njia ya simu yalimpatia kila mmoja fursa ya   kushinda. Kampeni hii ni uthibitisho kwamba huduma ya benki ya kidijitali inaweza kuwa ya kila mtu."

Benki pia ilihamasisha  wafanyakazi wake  katika matawi mbalimbali nchini  kuelimisha wateja, watumiaji wapya, na kutoa msaada wa kiufundi muda wote wa kampeni.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano , Nandi Mwiyombella alisema kampeni ya "Miamala ni Fursa” ilikuwa zaidi ya kujitangaza. “Tumewawezesha wateja si tu kwa zawadi za pesa taslimu, lakini pia kuwahakikishia pia wateja wetu kuwa huduma zetu za kidijitali ni zenye uhakika na wanaweza kuzitumia bila wasi”.

 Bank of Africa Tanzania inawashukuru washiriki wote na inampongeza mshindi   wa jumla wa zawadi kutoka Moshi, pamoja na washindi wengine wa kila wiki waliozawadiwa  kwa matumizi ya huduma za kidigitali zinazotolewa na benki.

Wakati benki inao mkakati wa kuleta kampeni za kunufaisha wateja siku za mbele,itaendeleza  dhamira yake kuongeza ujumuishaji wananchi katika sekta rasmi za kifedha na kuwezesha wananchi kunufaika na mapinduzi ya teknolojia na ya kidigitali.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda, amempandisha cheo Alphonce Simbu kutoka Sajini kuwa Sajinitaji katika hafla iliyofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya Jeshi Upanga Jijini Dar es Salaam leo Septemba 25, 2025 baada ya kupata mafanikio ya Mbio za Marathon Tokyo, Japan.

Jenerali Mkunda amesema ushindi wa Simbu wa kutwaa medali ya dhahabu katika Mashindano ya Mbio za Marathon ya Dunia Kilomita 42, zilizofanyika Toyo Japan ni kwa Watanzania wote na Afrika kwa ujumla na kwamba michezo ni sehemu ya kazi jeshini, hivyo Sajinitaji Alphonce Simbu amefanya kazi nzuri na kuwataka Maafisa na Askari wote jeshini kuiga mfano wa Sajinitaji Simbu.


Dr Ibrahim Shaddad met President for IUGS Dr Hassina Mouri is the President of the International Union of Geological Sciences (IUGS) Unesco chair in medical geology in Africa:


  • AMGC's Support: Encouraging more African states to join IUGS.
  • Medical Geology Cooperation: Exploring ways to work together on medical geology initiatives in Africa.
  • Upcoming Visit: Dr. Mouri is expected to visit AMGC in Dar es Salaam for further discussions and familiarization.

This potential partnership could lead to increased knowledge sharing, capacity building, and research in the field of medical geology, ultimately benefiting African nations.



..Yapongeza mchakato wa Ufungaji wa Mgodi wa viwango vya Kimataifa 

Na Mwandishi Wetu, 

Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) umeipongeza kampuni ya Barrick kwa weledi na kuzingatia viwango vya kimataifa katika mchakato wa ufungaji wa mgodi wake wa Buzwagi na kubadilisha matumizi ya eneo hilo na kuwa Kongani Maalum la Uwekezaji (SEZ) ambalo inafungua fursa za kiuchumi nchini.

Mjumbe wa maofisa hao wa TISEZA ukiongozwa na Mkurugenzi  Mkuu wake, Gilead John Teri ilifanya ziara hiyo kikazi jana na kuridhishwa na mchakato mzima wa ufungwaji wa mgodi huo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Bw.Gilead John Teri akizungumza na  Kamati ya Utekelezaji wa Kongani Maalum la Uwekezaji wa Buzwagi na Wafanyakazi wa Barrick baada ya kukamilisha ziara ya kikazi ya kutembelea eneo hilo.

Akiwa katika eneo hilo , Bw Teri alipata taarifa fupi ya uwekezaji wa aina mbalimbali ndani ya kongani hilo maalum la Uwekezaji (SEZ) na kukagua maeneo mbalimbali yatakayotumiwa na wawekezaji watakaohitaji kuwekeza katika Kongani hiyo na alitembelea kiwanda cha kuzalisha (Conveyor) ambacho tayari kimeanza kufanya uzalishaji na kutoa fursa za ajira.

Akiongea baada ya ziara hiyo,Bw.Teri alitoa pongezi kwa kampuni ya Barrick nchini kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za serikali kwa kufanikisha ufungaji wa mgodi huo kwa  viwango vya kimataifa na kufungua fursa ya eneo la kimkakati wa kukuza uchumi kupitia uanzishaji wa viwanda na kufungua milango ya biashara.

“Nawapongeza Barrick kwa kuhakikisha mgodi huu unafungwa kitaalamu pia nachukua fursa hii kuwashukuru kamati ya Utekelezaji wa Kongani hii inavyofanya kazi kwa Kushirikiana na mamlaka mbalimbali lengo likiwa kutimiza kufanikisha lengo la serikali la kuhakikisha eneo hili linatumika kimkakati ili liweze kuleta matokeo chanya kwa taifa ”,alisema Teri.

Teri pia alisema ameridhishwa na utangazaji wa eneo hilo unaoendelea ambazo zinabainisha fursa zilizopo na mipango iliyowekwa na serikali kwa ajili ya kutoa huduma kwa kuhakikisha zinapatikana katika eneo moja (One Stop Centre).

Kwa upande wake Meneja wa ufungaji wa Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi alisema tayari eneo hilo la kongani ya Buzwagi limepatiwa usajili na serikali kwa ajili ya shughuli hiyo maalum ambapo ukamilikaje wake utachochea ukuaji wa uchumi na ajira kwa vijana hapa nchini.

Meneja wa ufungaji Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi akifafanua jambo kwa ujumbe kutoka Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) jinsi mchakato  wa kubadilisha mgodi huo uliofungwa  kuwa  Kongani ya Buzwagi unavyoendlea  wakati ulipofanya ziara kwenye eneo hilo la mgodi.

Aidha Mumbi alieleza ujumbe huo kuwa hadi kufikia sasa wawekezaji  19 wameonyesha nia ya Kuwekeza katika Kongani hiyo huku wawekezaji tano  tayari wameanza mchakato wa usajili na tayari mwekezaji mmoja ameanza uzalishaji .

Hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,  Mboni Mhita, alitoa wito  kwa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) kuweka msisitizo katika kutangaza mradi mkubwa wa Kongani  Maalum la Uwekezaji wa Buzwagi ( SEZ) ambao unatarajiwa kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi kwa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Meneja wa ufungaji Mgodi wa Barrick Buzwagi, Mhandisi Zonnastral Mumbi (aliyenyoosha mkono)  akiwatembeza ujumbe kutoka Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya Kongani Maalum la Uwekezaji wa  Buzwagi.

Aidha,  RC Mboni alibainisha  kuwa Shinyanga ipo tayari kupokea wawekezaji kutokana na mazingira wezeshi yaliyowekwa na serikali pamoja na Mkoa kuwa na rasilimali zote muhimu kwa uwekezaji ikiwemo ardhi, upatikanaji wa maji, umeme, miundombinu ya kisasa ikiwa pamoja na barabara, uwanja wa ndege wa Shinyanga na Kahama, mtandao wa mawasiliano, na  nguvu kazi.

Meneja Utekelezaji wa Mradi  wa Kongani ya Buzwagi  kutoka Barrick, Stanley Joseph akifanya wasilisho kwa ujumbe wa maofisa waandamizi kutoka Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) uliofanya ziara mgodini hapo.

Ujumbe kutoka Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) ulipata fursa kutembelea maeneo ya wawekezaji mbalimbali kwenye eneo la Kongani Maalum la Uwekezaji wa Buzwagi.

Mwandishi Wetu, Beijing, China

Waandishi wa habari waandamizi kutoka Tanzania, Zimbambwe, Sudani Kusini, Ivory Coast and Uturuki wameshiriki mafunzo kwa vitendo nchini China hivi karibuni.

Mafunzo hayo yalihusu maendeleo ya teknolojia na mapinduzi yake ili kuleta matokeo chanya kwenye sekta ya habari na mawasiliano ya umma, na maendeleo ya taifa kwa jumla.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo  yaliyopewa kauli mbiu ya “Semina juu ya usimamizi wa vyombo vikuu vya habari katika nchi zilizo katika mpango wa ukanda na barabara” (Seminar on Senior Management of Mainstream Media in countries along the Belt and Road Initiative, -  ukanda mmoja na  njia moja ) Bw Augustino John Tendwa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) alisema mafunzo hayo yanayoendelea yamejikita katika kuleta fikira, ubunifu na matumizi ya kidigitaki katika kuleta mapinduzi ya tekolojia katika nchi za washiriki.

Afisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw Augustino John Tendwa (wa kwanza kulia) akishiriki kwenye mafunzo ya mapinduzi ya teknolojia yanavyoweza kuleta matokeo chanya kwenye sekta ya habari na maendeleo ya Tanzania kwa jumla.

Bw Tendwa alieleza kwamba washiriki wa mafunzo hayo ya vitendo walipata fursa ya  kutembelea makao makuu ya kampuni ya kimataifa ya teknolojia – Laird Technologies – kujifunza kwa vitendo maendeleo ya kiteknolojia yanayofanyika nchini China.

Wakiwa jijini Beijing, washiriki waliweza kujionea kwa karibu namna kampuni hiyo inavyoendesha uzalishaji wa vifaa vya hali ya juu vya kielektroniki, vikiwemo vifaa vya mawasiliano ya wireless, udhibiti wa joto, mitetemo na teknolojia ya kupunguza mwingiliano wa sumaku-umeme (EMI shielding).

Picha ya pamoja ikiwaonyesha maafisa habari kutoka Tanzania, Zimbambwe, Sudani Kusini, Ivory Coast and Uturuki wakihudhuria semina ya mafunzo kuhusu teknolojia inavyoweza kutumika kuleta maendeleo kwenye sekta za maendeleo kupitia vyombo vya habari na mawasiliano ya umma.

“Kampuni kama Laird ni mfano halisi wa namna China inavyowekeza katika ubunifu na utafiti wa kisayansi kwa ajili ya maendeleo ya teknolojia duniani. Hii ni fursa ya kujifunza na kutafuta maeneo ya ushirikiano kwa maendeleo ya sekta ya viwanda na teknolojia nchini kwetu,” alisema Bw Tendwa.

Aliongeza kwamba mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo waandishi na maafisa wa serikali kuhusu nafasi ya vyombo vya habari katika kuhimiza maendeleo kupitia ushirikiano wa kimataifa chini ya mpango wa ukanda na barabara.

Ushiriki wa Tanzania kupitia waandishi na maafisa waandamizi kutoka taasisi za serikali na vyombo vya habari ni ishara ya dhamira ya kukuza maarifa, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na atumizi ya teknolojia katika maendeleo ya taifa.














By Staff Writer,

Barrick, in partnership with the government of Tanzania , through its Bulyanhulu mine has continued improving primary education infrastructure environment by adding more classrooms at  Kharumwa English-medium school located in Nyang’hwale District in Geita region. This 

The project, which started on April 30, 2025, is expected to be completed on September 11, 2025.

This year, Nyang’hwale District Council has received Sh100,996,200 to implement the construction of four classrooms, and purchase furniture to address the challenge of classroom shortages.

Speaking at a ceremony to receive Uhuru Torch, which coincided with the laying of the foundation stone of the school, the Leader of Uhuru Torch Race, Mr Ismail Ali Ussi, commended Barrick Bulyanhulu for continuing supporting the government to improve people’s lives through the implementation of development projects in various sectors of the economy, including education.

Leader of Uhuru Torch race,  Mr. Ismail Ali Ussi (left), officially launches the laying of the foundation stone for the construction of classrooms for an English-medium school in Nyang’hwale District, Geita Region. On the right is the District Commissioner, Grace Kingalame.

“I take this opportunity to commend all experts of the Council and Barrick Bulyanhulu Mine for working day and night to ensure Tanzanians benefit from various projects which are implemented in this district,” Mr Ussi said.

Thus, he appealed to all Nyang’hwale residents to send their children to school. “There is no longer an excuse for long distances to school because schools are built everywhere and this is due to the collaboration of the Government and stakeholders like Barrick. Indeed, Barrick, you are supportive of Hon President Dr Samia Suluhu Hassan,” said Mr Ussi.

He explained further that the partnership shown by Barrick through its mines in the country is a clear indication of productive investment for the nation, and he urged other investors to emulate Barrick spirit by contributing to community development projects.

For her part, Nyang’hwale District Commissioner, Hon Grace Kingalame, stressed the importance of working hard and continuing with the spirit of implementing development projects at high standards to meet people’s needs.


Leader of the Uhuru Torch race, Mr. Ismail Ali Ussi, greets  Barrick Bulyanhulu employees shortly after the foundation stone laying ceremony for the construction of English-medium classrooms, an event that took place in Nyang’hwale District, Geita Region.

She emphasized that Barrick, through its Bulyanhulu mine, has been closely cooperating with them in all development projects for the broader interests of the country social wellbeing.

Barrick Representative at the event, Mr Samson Mashala, who is Community Relations Officer at Bulyanhulu Mine said the mine would continue working with the Government to ensure CSR projects were well-implemented to improve people’s lives. “This project is going to address congestion, and improve a study environment,” he said.

He added that the project has reached 85%  of its completion and will boost students' learning environment and contribute to positive outcomes in the education sector in the country.

The project, implemented through the force account system, is expected to reduce the problem of classroom shortages, overcrowding of students in classrooms, and promote a friendly learning environment.

 Na Mwandishi Wetu, 

Kampuni ya Barrick nchini yenye ubia na Serikali ya Tanzania, kupitia Mgodi wake wa Bulyanhulu imeendelea kuboresha mazingira ya elimu ya msingi kwa kuongeza ujenzi wa madarasa katika shule  ya mchepuo wa Kingereza ya Kharumwa iliyopo  Wilaya ya Nyang’hwale, Mkoa wa Geita. Shule hii imejengwa kwa fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR). 

Mradi wa kuongeza madarasa  ulianza Aprili 30, 2025, unatarajiwa kukamilika September 11, 2025.

Mwaka huu Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale imepata Sh100,996,200 kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa, na kununua samani kwa ajili ya kuondoa changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa.

Akizungumza wakati wa kupokea Mwenge wa Uhuru ulioambatana na kuweka jiwe la msingi katika shule hiyo hivi karibuni, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Bw Ismail Ali Ussi, aliipongeza Kampuni ya Barrick Bulyanhulu kwa kuendelea kuunga mkono jitihaza za Serikali za kuboresha maisha ya wananchi kupitia uwezeshaji wa miradi katika sekta mbalimbali, ikiwemo elimu.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Bw Ismail Ali Ussi (kushoto) akifungua uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa madarasa ya shule ya mchepuo wa kiingereza, Wilaya ya  Nyang’hwale, Mkoani Geita , kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Hiyo, Grace Kingalame.

“Nachukua fursa hii kuwapongeza wataalamu wote wa Halmashauri na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa kufanya kazi usiku na mchana katika kuhakikisha Watanzania wananufaika na miradi mbalimbali inayotekelezwa katika wilaya hii,” alisema Bw Ussi.

Hivyo, alitoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Nhang’hwale kuwapeleka watoto waso shuleni. “Hakuna tena kisingizio cha umbali mrefu wa shuleni kwa sababu shule zinajengwa kila sehemu na hii inatokana na ushirikiano wa Serikali na wadau kama Barrick. Hakika Barrick mnazidi kumheshimisha Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan,” alisema Bw Ussi.

Alifafanua kwamba ushirikiano unatolewa na kampuni ya Barrick kupitia migodi yake hapa nchini kiashiria cha uwekezaji wenye tija kwa taifa na kuwataka wawekezaji wengine kuiga mfano wa kampuni ya Barrick kwa kuchangia miradi ya maendeleo ya wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Nyang’hwale, Mhe Grace Kingalame alisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii na kuendelea na ari hiyo ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa viwango vya juu ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru, Bw Ismail Ali Ussi akisalimiana na wafanyakazi Barrick Bulyanhulu mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi wa ujenzi wa madarasa kwa mchepuo wa kiingereza tukio lilifanyika wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita .

Alisisitiza kwamba kampuni ya Barrick kupitia mgodi wake wa Bulyanhulu wamekuwa wakishirikiana kwa karibu katika miradi yote ya maendeleo kwa maslahi mapana ya Taifa.

Mwakilishi wa Barrick katika hafla hiyo, Bw Samson Mashala, ambaye ni Afisa Uhusiano wa Jamii katika Mgodi wa Bulyanhulu, alisema mgodi utaendelea kufanya kazi na Serikali kuhakikisha miradi ya CSR iliyoibuliwa na wananchi inatekelezwa kwa viwango na kuboresha maisha ya wananchi. “Mradi huu utaondoa shangamoto ya mrundikano wa wanafunzi katika darasa moja na kuboresha mazingira ya wanafunzi.”

Aliongeza kwamba mradi huo umefikia 85% ya ukamilishaji wake na utaongeza chachu ya wanafunzi kujifunza katika mazingira mazuri na kuchangia matokeo Chanya katika sekta ya elimu hapa nchini. 

Mradi umetekelezwa kwa mfumo wa force akaunti unatarajia kupunguza tatizo la madarasa, mrundikano wa wanafunzi wengi kwenye madarasa na kuchochea mazingira rafiki ya kujifunza.

Mwisho 

Na Mwandishi wetu-Arusha,

Kampuni ya Barrick yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga imetunukiwa  cheti cha tuzo  kwa kudhamini kikao kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma kilichomalizika  leo jijini Arusha.

Tuzo hiyo ilikabidhiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati , Dkt Dotto Biteko  ambaye alikuwa mgeni rasmi wa kufunga kikao hicho cha siku nne ambapo pia alitoa tuzo kwa taasisi nyingine zilizodhamini mkutano huo.


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mh. Dotto Biteko akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Bodi ya Twiga, bw.casmir Kyuki (kulia) baada ya kumkabidhi cheti cha udhamini (kushoto) ni Meneja wa Barrick nchini, Dkt.Melkiory Ngido.

Akiongea kuhusu udhamini huo kabla ya kukabidhiwa cheti cha tuzo,Meneja wa Barrick nchini Dkt.Melkiory Ngido alisema kampuni imedhamini kikao hicho kama mdau mkubwa wa maendeleo inayoamini kuwa sekta binafsi na Serikali zikishirikiana zinaweza kuleta  matokeo Chanya kwenye uchumi wa nchi kama inavyoonyesha kwenye Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025-2050.

Meneja wa Barrick nchini Dkt.Melkiory Ngido akiongea katika CEOs Forum kuhusu mafanikio yaliyopatikana kutokana na ubia wa Barrick na Serikali


Dkt.Ngido pia alisema kuwa Barrick imekuwa ikitekeleza falsafa ya 4R ya Rais Samia kwa vitendo ambayo imeleta ufanisi katika uendeshaji wa shughuli zake nchini kwa kushirikiana na Serikali ambapo imekuwa kioo cha uwekezaji wenye mafanikio nchini.

“Kupitia uwekezaji wetu na  uendeshaji wa shughuli zetu kwa ubia na Serikali tumepata mafanikio makubwa baadhi yake yakiwa ni kuwa kinara wa kulipa kodi na tozo mbalimbali ,kutoa gawio nono kwa Serikali,kunufaisha wazabuni wa ndani na kupanua wigo wa ajira kwa watanzania, matumizi ya teknolojia za kisasa  na kufanikisha miradi mikubwa ya kijamii hususani katika sekta za elimu,afya,miundombinu kupitia fedha za CSR zinazotolewa na migodi yake ya Bulyanhulu na North Mara”.

Dkt.Ngido pia alisema kuwa kampuni inaendelea kufanya tafiti mbalimbali za kijiolojia kwa lengo la utambuzi wa maeneo mapya ya uchimbaji na imeweza kurefusha maisha ya migodi yake kwa muda mrefu zaidi na kuendelea kunufaisha taifa.

Mwisho

Dar es Salaam, Tanzania -

Bank of Africa Tanzania joins diplomatic figures, business people, invited dignitaries and other cultural representatives to celebrate 26th anniversary of His Majesty King Mohammed VI’s accession to the throne of the Kingdom of Morocco as of its efforts to foster bilateral ties between Tanzania and Morocco.

Bank of Africa Tanzania proudly took part in the 26th anniversary celebration, the commemorative event, held in Dar es Salaam recently which among other things brought together distinguished delegates, diplomacy and other representatives to mark this important occasion.

Bank of Africa Tanzania is a subsidiary of the BANK OF AFRICA Group, a pan-African banking network headquartered in Morocco, with operations in 17 African countries and a strategic presence in France.

The Group is majority-owned by BANK OF AFRICA - BMCE, Morocco’s second-largest private bank. The bank reaffirmed its commitment to strengthening bilateral ties between Tanzania and Morocco through financial cooperation and cultural engagement.

The celebration underscored the growing relationship between the two nations, with Bank of Africa Tanzania standing as a bridge between East Africa and North Africa, fostering economic integration and shared prosperity.

Bank of Africa Tanzania remains committed to promoting regional development through strategic partnerships and impactful community engagement, in line with the group’s broader mission across Africa and beyond.

 The guest of honour was Hon. Ambassador Mahmoud Thabit Kombo (MP), Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation.

Staa wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa, Thierry Henry, ametangazwa rasmi kuwa balozi mpya wa kimataifa wa kampuni ya michezo ya kubashiri mtandaoni, Betway, wakati huu ambapo ligi kuu za barani Ulaya zinarudi dimbani kwa msimu mpya.

Thierry Henry 

Katika nafasi yake hiyo mpya, Henry anatarajiwa kuwa kiungo muhimu kati ya mashabiki wa soka na mchezo wenyewe, kupitia maudhui maalum na mitazamo ya kitaalamu atakayoshiriki kwa ushirikiano na kampuni hiyo.

Henry alianza soka lake la kulipwa nchini Ufaransa akiwa na AS Monaco, kabla ya kujiunga na Juventus kwa kipindi kifupi na kisha kutua Arsenal mwaka 1999, ambako alijizolea umaarufu mkubwa kwa kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu hiyo. Aliisaidia Arsenal kutwaa mataji mawili ya Ligi Kuu England (EPL), ikiwemo msimu wa ‘Invincibles’ mwaka 2003/04, na mataji matatu ya FA Cup.

Baadaye alijiunga na Barcelona, alikoshinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champions League) mwaka 2009 kama sehemu ya kikosi kilichotwaa mataji sita ndani ya msimu mmoja — rekodi ya aina yake barani Ulaya.

Katika ngazi ya kimataifa, Henry alikuwa sehemu ya kikosi cha Ufaransa kilichoshinda Kombe la Dunia mwaka 1998, na pia alitwaa taji la Euro 2000. Tangu astaafu soka, amekuwa kocha na mchambuzi maarufu wa soka katika vituo vya runinga mbalimbali.

“Soka siku zote limekuwa mchezo wa kasi na msisimko, na hayo ndiyo mambo ambayo Betway huwapatia mashabiki kwa namna ya kipekee,” alisema Henry. “Ninatarajia kushiriki kwenye kitu kikubwa kinachowaunganisha watu na mchezo wanaoupenda.”

Tangazo hilo limetolewa wakati ambapo Ligi Kuu England (EPL), La Liga na ligi nyingine kubwa barani Ulaya zinarejea, kipindi ambacho huwa na ushawishi mkubwa kwa mashabiki na wadau wa soka duniani kote.

Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni hiyo, uteuzi wa Henry unaonesha dhamira ya kuendelea kuwekeza kwenye soka la kimataifa. Betway tayari ni mshirika wa klabu kadhaa maarufu ikiwemo Arsenal, na inaendesha shughuli zake katika masoko mbalimbali ya Afrika, Ulaya na Amerika.

Mwisho

Utagharimu takribani  shilingi Bilioni 4.8 za kitanzania

Na Mwandishi Wetu, Kahama Shinyanga

Mgodi wa  Barrick Buzwagi ambao uko katika mchakato wa kufungwa  umefadhili mradi wa ujenzi wa chujio la maji ya mvua eneo la mwendakulima  wilayani Kahama mkoani Shinyanga unaoghalimu takribani shilingi Bilioni 4.8  kwa ajili ya kuwapatia wananchi wa mji wa kahama maji safi na salama.

Akiongea wakati wa hafla ya kupokea mwenge ulioambatana na kuweka jiwe la msingi la ujenzi huo wa mradi wa maji, Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Buzwagi ,Zonnastraal Mumbi alisema  mgodi katika hatua zake za mwisho za ufungaji umeamua kufadhili mradi huo ili kuondoa tatizo la upatikanaji wa maji kwenye Wilaya ya Kahama.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa , Ismail Ali Ussi (Mbele mwanzo kushoto) akikata utepe na uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa chujio wa maji ya mvua , mradi unaofadhiliwa na Barrick Buzwagi na serikali ya Tanzania eneo la mwendakulima Wilaya ya Kahama katika upokeaji wa mbio za mwenge leo mchana mjini Kahama , mwanzo kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda.

“haya ni matokeo ya ufungaji wa mgodi wa Buzwagi kwa kuamua kufadhili mradi mkubwa kabisa wa maji ya mvua kwa kutengeneza miundombinu ya uvunaji , ukusanyaji na usambazaji wa maji ya mvua kwa ajili ya matumizi wa wananchi wa mji ya Kahama,” alisema Mumbi.

Kiongozi wa Mbio wa Mwenge , Ismail Ali Ussi akihutubia hadhara na wageni waalikwa kwenye uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi katika mradi wa maji ya mvua eneo la mwendakulima.

Aliongeza kwamba moja ya dhamira ya kampuni ya Barrick inayoendeha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals ni kuunga mkono jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama.

Sehemu ya jiwe la msingi wa mradi wa ujenzi wa chujio wa maji ya mvua mjini kahama , shinyanga.

“Mgodi wa Buzwagi umefadhili mradi huu wa maji ya mvua kwa 62% kwa ajili ya kuhakikisha kwamba miundombinu ya kisasa na bora inajengwa kwenye mradi huu kama sehemu za kuleta matokeo Chanya kwa wananchi wa mji wa kahama,” alisisitiza

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na  Usimamizi wa Mazingira, , Mamlaka ya Maji Safi  wa Mazingira Kahama (KUWASA)Mhandisi , Magige Marwa , alitoa pongezi kwa kampuni ya Barrick nchini  kwa kufadhili mradi huo mkubwa ambao ukikamilika utaondoa changamoto ya upatikanaji maji safi na salama wilayani Kahama,


Aliongeza kwamba mradi wa ujenzi wa chujio la maji mwendakulima unatazamiwa kuhudumia zaidi ya 66% ya wakazi waishio manispaa ya Kahama na una uwezo wa kuzalisha lita milioni 10 kwa siku.

“Mradi huu unatarajiwa kukamilika Desemba mwaka huu na mpaka sasa 78% ya mradi mzima umeshakamilika kutokana na kasi ya ujenzi wa mradi huu mkubwa kwenye mji huu wa kahama,” alisisitiza

Mhandisi Marwa alifafanua kwamba mradi huo wa chujio la maji ya mvua 62% imefadhiliwa na mgodi wa Barrick- Buzwagi na 38% ni KUWASA kupitia Wizara ya Maji na Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.

Meneja wa Ufungaji wa Mgodi wa Buzwagi , Zonnastraal Mumbi wa pili kulia kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali.

Kwa upande wake , kiongozi wa mbio za mwenge , Ismail Ali Ussi alisema wizara ya maji inaendelea kufanya vizuri na kutekeleza kwa vitendo maono ya Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kumtua mama ndoo kichwani kwa kupeleka huduma ya maji mijini na vijijini.

 

Kiongozi wa mbio za mwenge, Ismail Ali Ussi (Katikati) akisikiliza maelezo ya mradi kutoka kwa msimamizi wa mradi huo ,  Mhandisi , Magige Marwa (wa kwanza kulia) ambaye ni Mkurugenzi wa Usambazaji Maji na  Usimamizi wa Mazingira, , Mamlaka ya Maji Safi  wa Mazingira Kahama (KUWASA) wa pili kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kahama , Frank Nkinda. 

“Nachukua fursa hii kuwapongeza wataalamu wote wa wizara na mamlaka za maji hapa kahama kwa kufanya kazi usiku na mchana katika kuhakikisha watanzania wanapata maji safi na salama,” amesema.

Sehemu ya ujenzi wa mradi wa maji ya mvua mwendakulima , Kahama shinyanga ndani ya mgodi wa Buzwagi Barrick.

Kwa upande wake , Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda alisisitiza kwamba umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii na kuendelea na ari hiyo ya kutekeleza miradi ya huduma za wananchi kwa viwango vya juu ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Mwisho

Author Name

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.